عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Stoneland, Rock city, Al-Hijr valley [Al-Hijr] - Swahili translation - Rowad Translation Center

Surah Stoneland, Rock city, Al-Hijr valley [Al-Hijr] Ayah 99 Location Maccah Number 15

Na hatukuuangamiza mji wowote ule isipokuwa ulikuwa na muda wake maalumu ulioandikiwa.

Isipokuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kilicho dhahiri.

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakayewakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua mno.

Na Mola wako Mlezi alipowaambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.

Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliyemuumba kutokana na udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umefukuziliwa mbali!

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakapofufuliwa.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika waliopewa muhula.

(Wataambiwa:) Ingieni humo kwa salama na amani.

Wape habari waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe zaidi, Mwingi wa kurehemu.

Isipokuwa watu wa familia ya Lut'. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.

Isipokuwa mkewe. Tumekwishapitisha kwamba huyo hakika atakuwa miongoni mwa watakaosalia nyuma.

(Lut') Alisema: Hakika nyinyi ni kaumu msiojulikana.

Ninaapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.

Na hakika miji hii ipo kwenye njia wazi inayopitiwa.

Kwa hivyo tukawaadhibu. Na hakika miji miwili hii iko kwenye njia iliyo wazi.

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji, Mwenye kujua zaidi.

Basi wewe yadhihirishe yale uliyoamrishwa, na jitenge mbali na washirikina.

Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanaofanya stihizai.

Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.

Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu, na uwe miongoni mwa wanaomsujudia.