عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Taha [Taha] - Swahili translation - Rowad Translation Center

Surah Taha [Taha] Ayah 135 Location Maccah Number 20

Twa Ha![1]

Arrahmani (Mwingi wa rehema), aliyeinuka juu ya Kiti cha Enzi.

Na ukinyanyua sauti kwa kusema, basi hakika Yeye anajua siri na chini zaidi kuliko siri.

Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu. Hakuna mungu isipokuwa Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na udumishe Swala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi.

Na nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?

(Musa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu.

Na mshirikishe katika jambo langu hili.

Na nimekuteua kwa ajili ya nafsi yangu.

Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tunaogopa asije akapindukia mipaka juu yetu au kufanya jeuri.

(Firauni) akasema: Basi Mola wenu Mlezi ni nani, ewe Musa?

Akasema: Elimu yake iko kwa Mola wangu Mlezi katika Kitabu. Mola wangu Mlezi hapotei wala hasahau.

Akasema: Miadi yenu ni siku ya Sikukuu ya mapambo; na watu wakusanywe kabla ya adhuhuri.

Basi wakazozana wenyewe kwa wenyewe kuhusiana na jambo lao hilo, na wakanong'ona kwa siri.

Kwa hivyo kusanyeni hila zenu zote, kisha mfike kwa kujipanga safu, na kwa yakini atafuzu kweli kweli leo atakayeshinda.

(Firauni) akasema: Oh! Mmemuamini kabla ya mimi kuwapa ruhusa? Hakika yeye ndiye mkubwa wenu aliyewafundisha uchawi huu. Basi kwa yakini nitawakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na lazima nitawatundika misalabani katika vigogo vya mitende, na hapo kwa yakini mtajua ni nani katika sisi ndiye mkali zaidi wa kuadhibu na kuiendeleza zaidi adhabu yake.

Hakika sisi tumemuamini Mola wetu Mlezi ili atusamehe makosa yetu na uchawi uliotulazimisha kuufanya. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mbora na Mwenye kudumu zaidi (katika kuadhibu).

Akasema: Hao wapo nyuma yangu wananifuata. Na nimefanya haraka kukujia, Mola wangu Mlezi, ili uridhike.

Na hakika Harun alikwishawaambia kabla yake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmetiwa mtihanini tu kwa kitu hiki. Na kwa yakini Mola wenu Mlezi ni Arrahmani (Mwingi wa rehema). Basi nifuateni mimi, na tiini amri yangu!

Na zitadhalilika nyuso mbele ya Aliye Hai milele, Msimamia yote milele. Na atakuwa ameharibikiwa mwenye kubeba dhuluma.

Kisha Mola wake Mlezi akamteua, na akamkubalia toba yake, na akamwongoa.

Na atakayeupa ukumbusho wangu mgongo, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa ni kipofu.

Aseme: Ewe Mola wangu Mlezi! Mbona umenifufua kipofu, nami nilikuwa nikiona vyema?

(Mwenyezi Mungu) atasema: Ndivyo hivyo. Zilikufikia ishara zetu, nawe ukazisahau; na vivyo hivyo leo utasahauliwa.

Na lau kuwa si neno lililokwishatangulia kutoka kwa Mola wako Mlezi na muda uliowekwa, bila ya shaka ingefika adhabu (duniani).