عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Ya Seen [Ya Seen] - Swahili translation - Rowad Translation Center

Surah Ya Seen [Ya Seen] Ayah 83 Location Maccah Number 36

Ya Sin.[1]

Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Wakasema: "Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu waliopindukia mipaka."

Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhahiri.

Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!

Jinsi Mola wangu Mlezi alivyonisamehe, na akanifanya miongoni mwa walioheshimiwa.

Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakachokitaka.

"Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.

Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu isipokuwa ni ukumbusho na Qur-ani inayobainisha.

Kwani mwanadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndiyo amekuwa ndiye mgomvi wa dhahiri!

Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakayeihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?