عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Sad [Sad] - Swahili translation - Rowad Translation Center

Surah Sad [Sad] Ayah 88 Location Maccah Number 38

Swad. Ninaapa kwa Qur-ani yenye ukumbusho.[1]

Mataifa mangapi tumeyaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita.

Na walisema: ‘Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hesabu.’

Na pia ndege waliokusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.

Na tukayafanya mashetani yamtumikie, wote wajenzi na wapiga mbizi.

Na hakika yeye kwetu Sisi ana cheo cha kukaribishwa kwetu, na pahala pazuri pa kurejea.

(Akaambiwa:) Piga-piga ardhi kwa mguu wako! Basi haya maji baridi ya kuogea na ya kunywa.

Na shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, kisha ndio upigie nacho, wala usivunje kiapo. Hakika tulimkuta mwenye subira, mbora wa waja, kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu.

Ndiyo hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marudio maovu kabisa;

Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia.

Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilichokuzuia kumtii yule niliyemuumba kwa mikono yangu? Je, umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?

Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakayofufuliwa viumbe.

Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa waliopewa muhula.

Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote.