عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The Pen [Al-Qalam] - Swahili translation - Rowad Translation Center

Surah The Pen [Al-Qalam] Ayah 52 Location Maccah Number 68

Nuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.[1]

Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.

Hakika Mola wako Mlezi ndiye ajuaye zaidi ni nani aliyeipotea njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.

Walitamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.

Wala usimtii kila mwingi wa kuapa, anayedharauliwa.

Mwenye kukejeli mno, anayetangatanga akieneza maneno ya kufitini.

Mkatili, na juu ya hayo, ni mshari aliyejipachika tu.

Wala hawakusema: Mwenyezi Mungu akipenda!

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.