The Noble Qur'an Encyclopedia
Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languagesThe earthquake [Al-Zalzala] - Swahili translation - Rowad Translation Center
Surah The earthquake [Al-Zalzala] Ayah 8 Location Madanah Number 99
Itakapotetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
Na itakapotoa ardhi mizigo yake!
Na mtu akasema: Ina nini?
Siku hiyo itahadithia habari zake.
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
Basi anayetenda chembe ya wema, atauona!
Na anayetenda chembe ya uovu, atauona!